Ubongo unaona matatizo akili inaona fursa kwenye hayo matatizo
Ubongo unaona matatizo akili inaona fursa kwenye hayo matatizo

Ubongo unaona matatizo akili inaona fursa kwenye hayo matatizo

๐พ๐‘–๐‘‘๐‘Ž ๐ผ๐‘๐‘Ÿ๐‘Žโ„Ž๐‘–๐‘šโœช

10 min
Comedy & Entertainment
Play

Description

<p>1 Mambo ya Nyakati 12:32<br /> โ€œNa wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.โ€</p> <p>Nataka uone hapa anaposema walikuwa watu wenye akili za kujua nyakati na kitu cha kufanya kwenye nyakati Kwanini? Kwa sababu ukisoma kile kitabu cha Mhubiri;</p> <p>Mhubiri 3:1-2<br /> โ€œKwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa;โ€<br /> Mungu alipanga vitu viende kwa muda na katika huo muda kuna vitu ambavyo tunatakiwa kufanya.<br /> MFANO<br /> Mungu alipomuumba mwanadamu pamoja na umuhimu wa magari hakutuumbia magari, na kwa sababu hiyo mwanadamu alipozaliwa na kuanza kutembea huku duniani kukosekana kwa barabara hakukuwa tatizo la kimaendeleo kwa nyakati zile, ubongo ulikuwa unaona kabisa kwamba hakuna barabara na akili ilikuwa inasema huna shida nayo. Lakini ikafika mahali muda unadai vitu viende kwa speed ndipo maswali ya usafiri yakaanza kuja na ndipo vikaja vyombo vya usafiri ili kurahisisha usafirishaji na mawasiliano na kurahisisha maendeleo kwenda kwa haraka. Sasa ilipofika mahali pa namna hiyo ubongo unapoona magari halafu hauoni barabara basi wenyewe (ubongo) unasema hili ni tatizo akili inasema hii ni fursa.</p> <p>Kwa hiyo ukitumia ubongo bila kutumia akili utalalamika.Ukitumia ubongo na akili utatafuta majibu ya changamoto na tatizo hilo.</p> <p>Ukiumwa jino kwako wewe unayeumwa jino ni tatizo lakini kwa daktari ni fursa. Ukiona garage zinajengwa wameona magari yanaharibika au wanatafuta fursa. Kama akili ikiwa kazini tafsiri ya vitu vilivyoko kwenye nyakati zilizoko zinakuwa tofauti kufuatana na nyakati. Ndio maana Mungu aliwaweka wana wa isakari wenye kujua nyakati na mambo yanayotakiwa yafanyike kwenye hizo nyakati nao walikuwa 200 na walikuwa viongozi wa ndugu zao. Mtu anayeweza kufikiri kesho yako kabla kesho haijafika uwe na uhakika atakuwa kiongozi wak

Uploader

daisy.road

daisy.road

Ubongo unaona matatizo akili inaona fursa kwenye hayo matatizo - Listen Free | WowFM