Nafsi na mwili viliumbwa vimilikiwe na roho
Nafsi na mwili viliumbwa vimilikiwe na roho

Nafsi na mwili viliumbwa vimilikiwe na roho

𝐾𝑖𝑑𝑎 𝐼𝑏𝑟𝑎ℎ𝑖𝑚✪

10 min
Comedy & Entertainment
Play

Description

<p>NAFSI NA MWILI VILIUMBWA VIMILIKIWE NA ROHO</p> <p>Zaburi 63:1<br /> “Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.”</p> <p>Mwandishi anamwambia Mungu, “Mungu wangu nitakutafuta mapema”, anaposema nitakutafuta ni roho ya Daudi inamweleza Mungu ya kwamba nitakutafuta mapema.</p> <p>Roho hiyo hiyo inasema kwa niaba ya nafsi, inasema nafsi yangu inakuonea kiu, lakini pia inasema kwa niaba ya mwili inasema mwili wangu wakuonea shauku.</p> <p>Nilitaka uone ya kwamba hauwezi kusema nafsi yangu kama haijapangiwa imilikiwe na roho na hauwezi kusema mwili wangu kama roho haikupangiwa kumiliki mwili.</p> <p>Ni dhambi iliyokuja na kukorofisha utaratibu wa uumbaji na mwili ukaonekana kama ndio unao tawala kila kitu, lakini Mungu aliweka kwa makusudi kabisa kwamba roho ya mtu ndiyo imiliki nafsi na mwili.</p> <p>AKILI IMO NDANI YA NAFSI</p> <p>Ayubu 32:8<br /> “Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.”</p> <p>Unganisha na kile kitabu cha Mwanzo ili uelewe vizuri zaidi:</p> <p>Mwanzo 2:7<br /> “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.”</p> <p>Kwa hiyo kama pumzi iliachilia nafsi ndani ya mtu na pumzi iliachilia akili ndani ya mtu kwa hiyo akili imo ndani ya nafsi.</p> <p>Akili tumeipata kwa msaada wa pumzi ya Mungu na nafsi tumeipata kwa msaada wa pumzi ya Mungu. Wakati nafsi inaingizwa ndani yetu na akili ziliingizwa, na ndiyo maana kama unayo nafsi lazima na akili unazo, hakuna mtu ambaye ameumbwa bila akili, ile kwamba huzitumii haina maana kwamba huna.</p> <p>AKILI SIO UBONGO, LAKINI MUNGU ALIVIUMBA VIFANYE KAZI KWA KUSHIRIKIANA</p> <p>Biblia ya Kiswahili inafundisha vizuri zaidi juu ya akili kuliko Biblia ya Kiingereza. Ukisoma Biblia ya Kiingereza unahitaji kuwa mwangalifu sana kutafuta neno akili kwa sababu limeandikwa kwa tafsiri tofauti tofauti kutegemeana na waliokuwa wakitafsiri na inategemea pia picha nzima ya habari inayozungu

Uploader

daisy.road

daisy.road

Nafsi na mwili viliumbwa vimilikiwe na roho - Listen Free | WowFM