
Kutumia Ubongo na akili kufanya maamuzi ya chanzo na matumizi ya pesa zako
๐พ๐๐๐ ๐ผ๐๐๐โ๐๐โช
Description
<p>UBONGO UNATAKIWA UKUSAIDIE KUWA NA MIPANGO YA KUPATA PESA LAKINI AKILI INATAKIWA ZIKUSAIDIE KUAMUA JUU YA CHANZO CHA KUPATA PESA NA KUAMUA MATUMIZI YA PESA HIZO</p> <p>Kazi mojawapo ya akili ni kutusaidia kupambanua mema na mabaya kwa jinsi ya Ki-Mungu ili tuweze kuchagua mema na kuacha mabaya. Biblia inatuambia kuwa akili zao kwa kutumiwa. haijasema kwa kutegemewa bali ni kutumiwa. Biblia imekataza kutegemea akili bali tunatakiwa tumtegemee Mungu.</p> <p>Shetani akitaka kuvuruga maisha yako atakamata akili zako maana ubongo unaweza kuwa na mipango mizuri sana ya kupata pesa lakini akili zako zisiwe vizuri katika kuangalia chanzo na matumizi ya pesa zako. Maana unaweza ukawa na mipango mizuri sana mbele ya watu au nchi lakini inaweza isikupe hela. Maana unaweza pata hasa sadaka ya shukrani ya kutoa jumapili katika hizo pesa zako. Lakini chanzo chako hakiko sawa maana kumbe hizo pesa umevunja benki mahali ukaiba.</p> <p>Fikiria mtu ambaye kaenda shule vizuri na kawa mhasibu mzuri na anapata mshahara mkubwa sana. Kitu cha kwanza anachofanya akiwa kazini anaanza kuiba. Sasa hapo kapata kazi kwa kutumia ubongo lakini akili zake haziko kazini na kwa sababu hiyo shetani anazitumia kumfanya aibe. Maana kama kaenda chuo na kapata cheti kwamba kasomea masuala ya accounting na Finance. Sasa badala ya kwamba kwa kuwa kasoma vizuri basi atumie ujuzi wake kuandika vizuri katika kutunza kumbu kumbu vizuri yeye anaandika asionekane kama kaiba pesa kumbe anaibia shirika au kampuni anayofanyia kazi.</p> <p>Lakini watu wa namna hii wanasema ni wizi wa kutumia akili. Lakini akili zimetumika vibaya na kumfanya mtu kwenda kuiba. Unahitaji kuwa na akili nzuri ambazo zinakuelekeleza kuwa hii njia ni sahihi lakini hii ni mbaya.</p> <p>Akili inakusaidia juu ya kutumia pesa hasa katika kuweka akiba.</p> <p>Mwanzo 41: 33-36<br /> Basi, Farao na ajitafutie mtu wa akili na hekima amweke juu ya nchi ya Misri. Farao na afanye hivi, tena akaweke wasimamizi juu ya nchi, na kutwaa sehemu ya tano katika nchi ya Misri, katika miaka hii saba
Uploader
Episodes
Kutumia Ubongo na akili kufanya maamuzi ya chanzo na matumizi ya pesa zako
๐พ๐๐๐ ๐ผ๐๐๐โ๐๐โช