Haijalishi unapitia hali gani na upo kwenye kipindi gani, Mungu yuko pamoja nawe
Haijalishi unapitia hali gani na upo kwenye kipindi gani, Mungu yuko pamoja nawe

Haijalishi unapitia hali gani na upo kwenye kipindi gani, Mungu yuko pamoja nawe

๐พ๐‘–๐‘‘๐‘Ž ๐ผ๐‘๐‘Ÿ๐‘Žโ„Ž๐‘–๐‘šโœช

10 min
Comedy & Entertainment
Play

Description

<p>Mtu aliyekuwa anatakiwa kwenye hii nafasi alitakiwa awe ana akili ya miaka 14 kusaidia Misri na nchi za jirani. Alitakiwa awe ana hekima pamoja na Roho wa Mungu ili kuweza kukamilisha jukumu hilo. Yusufu aligundua kuna kitu Farao alitakiwa akitolee nafasi (position) kwa sababu anaweza patikana mtu mwenye akili lakini asiwe na mahali pa kutumia akili zake.</p> <p>Kuna watu wana akili lakini hawana hekima na wengine wana hekima akili hawana. Yusufu alikuwa na hivyo vyote pia alikuwa na Roho wa Mungu ndani yake. Kwa maana hiyo Mungu alimpa nafasi ili aweze tumia akili, hekima na Roho ya Mungu iliyokuwa ndani yake katika kufanya alichotakiwa kufanya kwa miaka 14.</p> <p>Mwanzoni kabisa Yusufu aliotea ndoto akiwa na miaka 17 lakini alipewa kuwa waziri mkuu akiwa na miaka 30, kwa hiyo miaka 13 ilimtesa kufukia mahali pa kuweza kutumika miaka 14. Kwa sababu alipitia wakati mgumu sana miaka hiyo 13 maana Mungu alimleta duniani kwa kazi hizo kubwa. Moja ya kazi ni kuhakikisha ile miaka 14 pale Misri akili zake zinatumika sawasawa kwa sababu alisema</p> <p>Mwanzo 45:7โ€ญ-โ€ฌ8<br /> โ€œMungu alinipeleka mbele yenu kuwahifadhia masazo katika nchi, na kuwaokoa ninyi kwa wokovu mkuu. Basi si ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri.โ€</p> <p>Maana yake amekuwa na akili iliyomfanya kuwa baba kwa Farao mahali ambapo kwa jinsi ya kawaida isingewezekana pia akawa baba kwa taifa la Misri na kwa ndugu zake. Yusufu ndoto (vision) yake ilikuwa ya contract ya miaka 14. Lakini alifanya vizuri kiasi ambacho hakustaafishwa baada ya muda wake kuisha bali aliendelea na kazi mpaka alipo kufa.</p> <p>Kumbuka Yusufu alipewa akili ya kusaidia ndugu zake lakini ndugu zake walimkataa hata alipoenda kuwapelekea chakula walipomwona walimkasirikia wakaanza kupanga kumu ua. Sasa fikiria walitaka kuua akili ya namna gani kwa kubebeshwa kitu cha aina gani. Kwa hiyo ili wasimuue wakakubaliana kumtumbukiza kwenye kisima kisicho na maji halafu wakafikiria

Uploader

daisy.road

daisy.road

Haijalishi unapitia hali gani na upo kwenye kipindi gani, Mungu yuko pamoja nawe - Listen Free | WowFM