
Uko mahali kwenye maisha yako kila kitu kimesimama, Yesu anakutafuta
𝐾𝑖𝑑𝑎 𝐼𝑏𝑟𝑎ℎ𝑖𝑚✪
Описание
<p>Hii unaweza ukasikia mtu akisema “nimemlea huyu mtoto nikifikiri akili anazo kumbe hana”. Ukishasikia lugha ya nmna hiyo ina maana akili hazifanyi kazi inayotakiwa kwa sababu hamna mtu ambaye hana akili ila kuna namna zimebanwa.</p> <p>Sasa angalia yule kijana wa nchi ya Wagerasi kila mtu alikuwa kamkatia tamaa. Sasa Yesu alikuwa hafanyi jambo lolote isipokuwa kamuomba baba akifanya. Kwa hiyo walikuwa anafanya mapenzi yake maana alikuwa akimuona Yesu kayakamilisha. Yesu aliposema tuvuke mpaka ng’ambo ina maana aliuacha mkutano mkubwa alafu akaingia katika boti kwenda ng’ambo mpaka nchi ya Wagerasi. Wanafunzi wake walikuwa hawajui wanaenda kufanya nini huko lakini Roho Mtakatifu alikuwa anajua kwamba kuna mtu yupo makaburini hapati hata msaada maana tunaona hakupelekwa na watu kwa Yesu.</p> <p>Maandiko yanatuambia kuwa Yesu alipofika tu alianza kukemea mapepo na ndio maana yalianza kupiga kelele kuwa tuna nini na wewe Yesu. Yesu alimfuatilia yule kijana maana tunaona hamna mtu aliyempeleka kwa Yesu kwa sababu kulikuwa na mkutano ng’ambo ya ziwa kwa sababu wangekuwa na haja ya kumpeleka wangempeleka kwa Yesu alipokuwa ng’ambo maana boti zilikuwepo za kuweza kuwavusha hata ng’ambo ya pili. Kila mtu alikuwa amemuacha na hapati msaada hata ndugu zake hawakumsaidia.</p> <p>Unisikilize inawezekana kabisa uko mahali na kila kitu chako kimekwama, nipo hapa kukuambia neno la Bwana kuwa Yesu yupo ng’ambo na atakuja kukufuata na wewe ili aje kukutembelea. Haijalishi maisha yako yako mahali pagumu kiasi gani kama vile makaburini Yesu atakuja yeye mwenyewe kukufuata hata kama haujakaribishwa kwenye mkutano.</p> <p>Yesu alipomfuata yule kijana alihusika moja kwa moja na akili zake maana alijua kabisa ya kwamba yule kijana akifunguliwa akili tu anaweza akasimama peke yake. Yule kijana alipoponywa biblia inatuambia alivaa nguo. Sasa swali linakuja hizo nguo alizipata wapi? Kwa hiyo inawezekana kabisa hakuchana nguo zote bali alikuwa anavua kila akivalishwa. Maana hatuoni kama kuna mtu alimpa nguo hata watu wa pale maana
Загрузчик
Эпизоды
Uko mahali kwenye maisha yako kila kitu kimesimama, Yesu anakutafuta
𝐾𝑖𝑑𝑎 𝐼𝑏𝑟𝑎ℎ𝑖𝑚✪