
Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya pili)
๐พ๐๐๐ ๐ผ๐๐๐โ๐๐โช
Deskripsi
<p>Katika siku hizi za mwisho ambazo Yesu anakaribia kurudi dunia lazima ijue, mkubwa kwa mdogo lazima wajue kwamba kurudi kwa Bwana kumekaribia. Biblia inasema na watakatifu na wazidi kujitakasa, wanaofanya kazi ya Mungu na wafanye upesi maana Roho pamoja na malaika na watumishi wanasema njoo, maana yake kuna kitu kinachomzuia asije.</p> <p>Biblia inasema injili ya Ufalme wa Mungu itakapohubiwa kote, anasubiri tufanye kazi yake. Kama umesoma kitabu cha Luka wakati Yesu amefufuka</p> <p>Luka 24:44<br /> Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya. Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu. Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki. Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.</p> <p>Matendo ya mitume inasema malaika waliokuwepo pale wakawaambia wale watu kuwa kwa jinsi wanavyomwona anaenda ndivyo watakavyomwona anarudi.</p> <p>Kabla ya kuwaahidi Roho Mtakatifu aliwafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Kwa sababu unaweza ukawa na Roho Mtakatifu na usielewe maandiko kwa sababu Roho Mtakatifu anahitaji ushirika wa akili, kuonyesha kwamba Roho Mtakatifu anapoingia kazini lazima akili ziwe active. Kwa sababu huko ndiko kunakoelewa.</p> <p>Imani inaweza kukufanya kuchukua hatua ya kitu ambacho huelewi kwa sababu huwezi kuelewa kila kitu ambacho Mungu anakuambia fanya, vingine inahitaji kuchukua hatua kwa imani, lakini pia kudumu katika hicho alichokufanyia unahitaji kudumu katika Neno kwa sababu mtu hakuitwa kuishi kwa muujiza bali kwa Neno linalotoka katika pumzi ya Mungu.</p>
Pengunggah
Episode
Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya pili)
๐พ๐๐๐ ๐ผ๐๐๐โ๐๐โช