Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho
Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho

Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho

๐พ๐‘–๐‘‘๐‘Ž ๐ผ๐‘๐‘Ÿ๐‘Žโ„Ž๐‘–๐‘šโœช

10 min
Comedy & Entertainment
Putar

Deskripsi

<p>Na Biblia inasema Yesu siku za mwisho hatakuja hapa duniani, kwa sababu maandiko yanasema kile kiti cha enzi kikubwa cheupe, kiti cha hukumu dunia itakimbia na mbingu zitakimbia na kwa sababu hiyo hicho kiti hakitakuwa duniani kwa sababu dunia itakimbia na mbingu zitakimbia. Biblia inasema nikawaona wafu wakubwa kwa wadogo wamesimama katika kiti cha enzi halafu atasimama pale kama hakimu. Sasa hivi ni mwokozi wako lakini ukikutana naye ngโ€™ambo ya pili kama hujaokoka utakutana naye kama hakimu na maandiko yanasema atabagua na kuita majina. Biblia inasema mauti itaitwa iwatoe wafu, bahari na kuzimu itaitwa.</p> <p>Unajua saa nyingine tunafanya kazi ya Mungu tunasahau kuwaambia na kuwahimiza watu juu ya ukaribu wa kurudi kwa Yesu.</p> <p>Tangu watoto wetu wakiwa wadogo kati ya kitu ambacho tumekuwa tukiwasemesha mara kwa mara ni hiki. **Kwenye mambo ya rohoni waishi kama watakufa sasa hivi, na kwenye mambo ya mwilini waishi kama vile hawatakufa maana yake kwenye mambo ya rohoni waishi wakiwa tayari Yesu akishuka sasa hivi wawe tayari, hawana shida ya kutahayari wanaenda pamoja na Bwana, lakini waendelee kupanga maisha yao na kufanya shuguli zao na kupanga mambo mbalimbali kama vile kufa hakupo. **</p> <p>Na watu wengi wanapanga mambo yao kama vile Yesu hatatokea wakati wowote ule. Na kitu mojawapo katika utumishi ukishapoteza sura ya kurudi kwa Yesu uwe na uhakika utapoteza na uchaji na utapoteza umuhimu wa nyakati, utataka kufanya vitu vyako saa yeyote unayotaka lakini huwezi kufanya kazi ya Mungu saa yeyote unayotaka, huwezi kutii kitu cha Mungu saa yeyote unayotaka.</p> <p>Mungu ameachia kila kitu kwa saa yake na mipango yake na anategemea watu wake sio tu watii Neno lake lakini watii Neno lake katika nyakati na muda aliowawekea kwa sababu nyakati na muda aliowawekea ndizo zinazoweka thamani ya Neno.</p> <p>Jaribu kuzungumza na mtu ambaye hajaokoka kabla hajafa halafu ukasema nina shughuli nyingi halafu kesho ukamkuta amekufa, thamani ya Neno lako la wokovu kwa yule mtu imepotea, lilikuwa na thamani jana alip

Pengunggah

daisy.road

daisy.road

Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho - Listen Free | WowFM