
Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Tatu)
𝐾𝑖𝑑𝑎 𝐼𝑏𝑟𝑎ℎ𝑖𝑚✪
विवरण
<p>Kwa hiyo tangu wakati ule kuna vitu ambavyo alivyokuwa anafanya moja kwa moja vinazaa tena mfano wa kile kitu alichobeba. Sasa unaweza ukaelewa kwa nini katika kipindi hiki cha Agano jipya ni lazima tuzaliwe kwa mara ya pili.<br /> Maandiko yanatuambia ndani yake tunaishi, tunakwenda na kuwa na uhai wetu na Biblia inatuambia tutaishi kwa imani Ni imani ya namna gani? Waebrania anasema<br /> Waebrania 11:6<br /> “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.”</p> <p>IMANI YA KWANZA NI HII:-<br /> PASIPO IMANI HAIWEZEKANI KUMPENDEZA; KWA MAANA MTU AMWENDEAYE MUNGU LAZIMA AAMINI KWAMBA YEYE YUKO<br /> Yaani usiishi kama vile Mungu hayupo. Kwenye Kiswahili cha kawaida tunahiita Uchaji Kwenye tafsiri nyingine ya kiingereza inaitwa hofu ya Mungu The fear of God. Kujua ya kwamba Mungu yupo.<br /> Kwa sababu ile tu kujua ya kwamba Mungu yupo inatosha kubadilisha na kuweka msimamo wako na malengo yako kwa namna ambavyo unajua Mungu yupo.</p> <p>IMANI YA PILI NI HII:-<br /> KILA AMWENDEAYE MUNGU LAZIMA AAMINI KWAMBA YEYE YUKO, NA KWAMBA HUWAPA THAWABU WALE WAMTAFUTAO<br /> Kwa nini tunamtafuta? kwa sababu dhambi ilitutenga naye.</p> <p>AINA NYINGINE YA IMANI NI KWENYE KITABU CHA<br /> Waebrania 11:1<br /> “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.”</p> <p>Kwa sababu dhambi ilipoingia ilituvurugia mawasiliano yetu ya kawaida na vitu visivyoonekana na ulimwengu wa roho. Maana ilikuwa ukienda kwenye ulimwengu wa roho ni au Mungu ajifunue kwako la sivyo utakutana na ulimwengu wa roho wa ulimwengu wa giza na ndiyo maana wanadamu ni wepesi sana kushabikia vitu vya ulimwengu wa giza kuliko vile vya ulimwengu wa nuru, kwa sababu hivyo vya giza ndiyo mazingira tuliyonayo. Shetani anajiita mungu wa dunia hii na katengeneza mazingira ambayo ni kitu cha kawaida huoni watu wakishtuka watu wakienda kwenye nguvu za giza, lakini watashtuka wakisikia kwenye familia mtu akiokoka.<br /> Imani i
अपलोडर
एपिसोड
Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Tatu)
𝐾𝑖𝑑𝑎 𝐼𝑏𝑟𝑎ℎ𝑖𝑚✪